Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment and dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment and dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment., dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment., dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!!

Waziri mkuu MAJALIWA asema hataruhusu wanasiasa kusababisha vurugu

Waziri mkuu MAJALIWA asema hataruhusu wanasiasa kusababisha vurugu:;              

Waziri Mkuu KASSIM MAJALIWA amesema Serikali itahakikisha inalinda amani iliyopo nchini gharama yoyote ile na kamwe haitoruhusu mwanasiasa yeyote                                   
Waziri Mkuu KASSIM MAJALIWA amesema Serikali itahakikisha inalinda amani  iliyopo nchini gharama yoyote ile  na kamwe haitoruhusu mwanasiasa yeyote kusababisha vurugu zitakazochochea uvunjifu wa amani.
Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na viongozi wa dini pamoja na wazee wa mkoa wa RUKWA baada ya kuwasili mkoani humo kwa ziara ya kikazi ya siku mbili. 
Waziri Mkuu  KASSIM MAJALIWA amesema  serikali inataka Watanzania waweze kufanya kazi zao zinazowaingizia kipato na kuwaletea tija katika hali ya utulivu hivyo suala la kudumisha amani ni muhimu kwani vurugu zikitokea hawatakuwa na mahali pa kukimbilia
Waziri Mkuu amewataka viongozi wa dini kuendelea kuliombea Taifa pamoja na viongozi wake kwa sababu kazi ya uongozi ni ngumu na ina changamoto nyingi.
Hali kadhalika Waziri Mkuu MAJALIWA  amewaagiza viongozi wa dini wa mkoa wa RUKWA kuharakisha uundwaji wa Kamati ya Amani ya mkoa huo.
Naye Sheikh wa mkoa wa Rukwa, Rashid Akilimali amesema madhehebu ya dini hayawezi kuvuruga amani ya nchi ila anahofu na baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa kutokana na vitendo vyao vya kuhamasisha vurugu.
Kwa upande wake Katibu wa Wazee mkoani Rukwa, Kanali Mstaafu, JOHN MZURIKWAO amemuomba waziri mkuu kuwasaidia  kutatua kero mbalimbali zinazoukabili mkoa huo zikiwemo za malipo ya pembejeo kwa mawakala wa kilimo pamoja na mgogoro wa Ardhi katika shamba ya Efatha.
Share And Comment Bellow On What You Think About This Post!!!

Comments

Facebook Twitter Youtube