Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment and dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment and dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment., dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment., dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!!

Taasisi ya Moyo ya JAKAYA KIKWETE Yafanikisha Upasuaji wa Moyo kwa Wagonjwa 6 Bila ya Kutumia Mashine..:;

                  
Taasisi ya Moyo ya JAKAYA KIKWETE – JKCI iliyopo Jijini Dar es salaam kwa kushirikiana na timu ya wataalamu kutoka hospitali ya APOLLO ya nchini INDIA imefanikiwa kufanya upasuaji kwa wagonjwa wa moyo Sita bila kutumia mashine ya mapafu na moyo.

Akizungumza na waandishi wa habari Jijini DAR ES SALAAM kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi  hiyo, mmoja wa madakta wa taasisi hiyo Dkt. BASHARI  NYANGASA amesema kuwa upasuaji huo umesahidia kupunguza madhara ambayo yangetokana na kutumia  mashine hizo.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa tiba ya moyo Dkt. PETER KISENGE amesema kuwa upasuaji wa aina hiyo ni ni endelevu na kutoa wito kwa madaktari wote nchini kuwapeleka wagonjwa wenye matatizo ya moyo  katika taasisi hiyo ili wakapatiwe  matibabu.

Upasuaji huo kwa wagonjwa wa moyo SITA ndani ya nchi umeisaidia serikali kuokoa zaidi ya Shilingi Milioni 170 ambazo zingetumika endapo wagonjwa hao wangetibiwa nje ya nchi. 



COMMENT AND SHARE.................!!!!!!
Share And Comment Bellow On What You Think About This Post!!!

Comments

Facebook Twitter Youtube