Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment and dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment and dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment., dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment., dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!!

Wizara Kilimo, Mifugo na Uvuvi yaagizwa kufufua sekta ya ushirika

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akifurahia picha yake iliyochorwa na kutolewa kwake na Chama cha Waandishi wa Habari za Utalii na Uwekezaji Tanzania mkoani Mbeya (TAJATI) katika Kilele cha sherehe za Maonyesho ya wakulima Nanenane zilizofanyika kwenye Uwaja wa John Mwakangale, jijini Mbeya jana. Wa tatu kutoka kulia kwake ni mkewe Mary, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla (katikati), wanachama wa chama hicho na maofisa mbalimbali. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)                 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameiagiza Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kuhakikisha inafufua sekta ya ushirika na kuwachukulia hatua kali watendaji wote waliohujumu ushirika na kusababisha machungu kwa wanaushirika ili iwe fundisho kwa wengine.
Pia ameitaka wizara hiyo kupitia upya sekta ya ushirika kwa kuanza na viongozi walipo ndani ya wizara hadi mikoani kuhakikisha kama wanafanya kazi zao ipasavyo na kuwaondoa watakaobainika kwa uzembe.
Waziri Mkuu alitoa agizo hilo jana wakati akifunga maadhimisho ya Sherehe za Wakulima Nanenane kwa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, yaliyofanyika kwenye Uwanja wa John Mwakangale mkoani Mbeya.
Alisema mkulima, mfugaji na mvuvi mdogo au mmoja mmoja hawezi kupunguza umasikini bila ya kuwa na chombo cha kuwaunganisha na kuwapa nguvu ya kutetea bei ya mazao yao kama ushirika. Aidha alisema ushirika imara utawasaidia kutafuta soko na kupata mikopo ya riba nafuu.
Alisema pamoja na umuhimu wa kuwepo kwa ushirika, tasnia hiyo imewaumiza wakulima wengi na kuwafanya kukata tamaa katika uzalishaji kutokana na usimamizi mbovu, ubadhirifu na ubabe wa baadhi ya viongozi wa ushirika.
“Wahimizeni na kuwashawishi wakulima, wafugaji na wavuvi kujiunga katika vikundi vya ushirika vya uzalishaji na Saccos. Aidha, elimu ya ushirika inayotolewa kwenye maonesho ya mwaka huu, iwe changamoto kwenu kwamba umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu,” alisema.
Wakati huo huo, Waziri Mkuu alisema Serikali haitamvumilia mfugaji anayelisha katika maeneo ya hifadhi na vyanzo vya maji na aliwataka wakuu wa mikoa na wilaya waendelee kulinda maeneo hayo.
Kwa upande wake Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, William ole Nasha alisema sekta ya kilimo imekuwa na mafanikio makubwa ambapo katika kipindi cha miaka minne mfululizo nchi imeweza kuzalisha chakula cha ziada, ambapo kwa mwaka huu imezalisha kwa asilimia 123.
“Mafanikio hayo yanachangiwa na jitihada za Serikali katika kutoa ruzuku ya pembejeo, taasisi za utafiti ambazo zimekuwa zikitafiti aina bora ya mbegu zikitafuta mbegu bora na wakulima walioamua kuwekeza kwenye kilimo,” alisema.
Naibu Waziri Ole Nasha alisema katika ukanda wa Nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ni nchi mbili tu za Tanzania na Zambia kati ya nchi 15 za jumuiya hiyo, hazikabiliwi na baa la njaa.
Mwenyekiti wa Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Tanzania (Mviwata) Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Ladislaus Mwanakatwe aliipongeza Serikali kwa jitihada zake za kuwatetea pamoja na utatuzi wa kero za muda mrefu zilizokuwa zinawakabili wakulima ikiwemo ya tozo.
Share And Comment Bellow On What You Think About This Post!!!

Comments

Facebook Twitter Youtube