Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment and dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment and dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment., dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment., dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!!

SIMBA yamuita MO Mezani

            
UONGOZI wa klabu ya Simba umemwandikia barua mfanyabiashara Mohamed Dewji, ‘Mo’ kutaka kujadiliana naye juu ya nia yake ya kununua hisa asilimia 51 za klabu hiyo kwa Sh bilioni 20.
Katika barua yake hiyo iliyoandikwa na Katibu Mkuu wa Simba, Patrick Kahemele ilimtaka Mo kuwasili Agosti 15 katika Hoteli ya Serena kwa ajili ya majadiliano hayo na Kamati ya Utendaji.
Mo ambaye aliwahi kumiliki timu za African Lyon pamoja na Singida United, ameonesha nia ya kununua hisa hizo jambo linaloonekana kuwavutia wanachama wengi wa klabu hiyo.
Juzi katika Mkutano Mkuu wa wanachama uliofanyika Bwalo la Maofisa wa Polisi Oysterbay, hoja kubwa ilioonekana kuutawala mkutano huo ni uuzwaji wa hisa hizo ambapo ilisababishaa wanachama kuvuruga kujadiliwa kwa hoja nyingine.
Wanachama wengine wakiwa wamevalia fulana zisemazo ‘Mpeni Mo timu yake’ huku wengine wakipiga kelele wakilitaja jina la Mo, walizua tafrani hali iliyosababisha rais wa klabu hiyo, Evans Aveva kuahirisha ujadiliwaji wa hoja nyingine na kusisitiza kuwa hoja ya mabadiliko imekubaliwa na kuwa timu hiyo inaanza mchakato wa uendeshwaji katika mfumo wake mpya.
Baada ya hoja hiyo, jana asubuhi Mo alifanya mkutano na waandishi wa habari ofisini kwake akiweka wazi kuwa ameshaandika barua rasmi ya kutaka kununua hisa hizo huku akiwapa miezi mitatu Simba kumpatia jibu.
Mo alisema amekuwa na nia ya kununua hisa muda mrefu kwa kuwa akiwa kama mwanachama wa klabu hiyo anaona kuwa kuna udhaifu mkubwa kwa sasa ambao unatakiwa kukabiliwa.
Saa chache baada ya mfanyabiashara huyo ambaye ni kati ya wafanyabiashara vijana wakubwa barani Afrika kumaliza mkutano wake huo, Simba ilituma barua kwa vyombo vya habari inayoelezea kumuita kikaoni Mo.
Barua hiyo ilisema kuwa imeamua kumwita kikaoni Agosti 15 kwa kuwa wiki ya kwanza ya mwezi huu klabu hiyo itakuwa na shughuli nyingi za kufanya na hasa maandalizi ya Simba day inayotarajiwa kufanyika Agosti 8. Pia ilifafanua kuwa kwa sasa inashughulikia usajili na hivyo kuongeza kuwa ina imani kuwa tajiri huyo atafika kwa kikao Agosti 15.
Mo katika kikao chake za asubuhi alisema kuwa kwa sasa anachotaka ni kuona maendeleo ya Simba na sio vinginevyo na kuongeza kuwa akipewa nafasi atahakikisha anawekeza fedha, muda na mapenzi yake yote kwa klabu hiyo.
Share And Comment Bellow On What You Think About This Post!!!

Comments

Facebook Twitter Youtube