Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment and dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment and dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment., dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment., dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!!

Wilaya ya Makete Kupiga Mrufuku Ulaji wa Nyama ya Nguruwe, Sababu Yatajwa

 



Halmashauri ya Wilaya ya Makete mkoani Njombe imepiga marufuku Watu kuchinja Nguruwe na kula nyama yake (kitimoto) kwa muda usiojulikana kutokana na taarifa za uwepo wa ugonjwa wa homa ya nguruwe.

Afisa Mifugo na Uvuvi wa Wilaya hiyo Aldo Mwapinga ametoa taarifa ya katazo hili kutokana na vifo vya nguruwe 21 Wilayani humo na amenukuliwa akisema “Kata ya Tandala kumeripotiwa dalili za ugonjwa wa homa ya Nguruwe kwahiyo tunaendelea na jitihada za kuhakikisha tunashirikiana na Watendaji kuanzia ngazi ya Kata hadi Vitongoji kutoa taarifa juu ya hali inavyoendelea”

Amesema Serikali imepiga marufuku hiyo hususani katika kata ya Tandala huku pia akizuia utoaji wa Nguruwe kutoka kwenye zizi moja kwenda jingine kwa ajili ya kupandisha kwa jike, vilevile amewataka Watu kuacha kufukua Nguruwe waliofukiwa baada ya kufa (mizoga) na kuwachinja kisha kwenda kuuza nyama hizo vilabuni nyakati za usiku, hii ni baada ya taarifa za namna hiyo kuripotiwa hivi karibuni. 

Share And Comment Bellow On What You Think About This Post!!!

Comments

Facebook Twitter Youtube