Urusi: Tumechoshwa na madai ya Marekani Kuhusu Sisi..:;
on
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
Urusi inasema kuwa madai kuwa
Marekani iliendesha kampeni ya udukuzi wa mitandao ili kushawishi
uchaguzi wa urais nchini Marekani si kweli.
Msemaji wa serikali ya Urusi Dmitry Peskov aliwaambia waandishi wa habari kuwa Urusi imechoshwa na madai hayo.
Alisema kuwa ripoti iliyotolewa na mashirika ya ujasusi nchini Marekani kuhudu madai hayo haina msingi wowote.
Hayo ndiyo matamshi ya kwanza kutoka Urusi tangu rais mteule Donald Trump akabidhiwe ripoti hiyo.
Trump amekuwa akipinga madai ya udukuzi wa Urusi tangu ashinde uchaguzi wa urais mwezi Novemba.
Lakini mkuu wake wa jeshi Reince Priebus, amesema kuwa Trump
amekubali matokeo ya uchaguzi ambayo yaliwasilishwa kwake na wakuu wa
ujasusi.
"Hajakana kuwa urusi ilihusika kwenye masuala fulani," Priebus alisema.
Hata hivyo hakufafanua ikiwa Trump aliamini ripoti kuwa rais wa Urusi Vladimir Putin alikuwa ameamrisha udukuzi huo kufanyika.
Bwana
Trump alitaja mkutano wa Ijumaa na wakuu wa ujasusi kuwa wenye manufaa,
na kusema kuwa ataomba kati kipindi cha ndani ya siku tisini ofisini,
kufanyika mpango wa kuzuia udukuzi wa mitandao.
COMMENT AND SHARE.................!!!!!!!!
Share And Comment Bellow On What You Think About This Post!!!
Comments
Post a Comment
Welcome.......
What are you thinking of....!!