Wanamgambo wa kundi la al-Shabab
wamewaua kwa kuwapiga risasi watu watatu kusini mwa Somalia, wawili kati
yao kwa makosa ya kushiriki mapenzi ya jinsia moja.
Mwanamume wa tatu aliuawa kwa kufanya ujasusi dhidi ya kundi hilo.
Sheikh
Mohamed Abu Abdalla, gavana mwanachama wa al-Shabab alisema Isak
Abshirow, 20, na Abdirizak Sheikh Ali, 15, walifumaniwa na wapiganaji wa
al-Shabab wakifanya mapenzi.
Wanaaminika kuwa watu wa kwanza kuuawa na al-Shababkwa makosa ya kushiriki mapenzi ya jinsia moja.
Saeed
Mohamed Ali alipatikana na kosa la kufanyia ujasusi vikosi vya Ethiopia
ambao ni sehemu ya kikosi cha wanajeshi wa Muungano wa Afrika
wanaokabiliana na wanamgambo hao.
Wanaume hao waliuawa hadharani na katika mji Buale ambako umati mkubwa wa watu ulikuwa umekusanyika.
Mtandao
mmoja ulio na ufungamano na kundi hilo, umeripoti kuwa mahakama ya
Kiislamu katika eneo la Jubba iliwapata wanaume hao na hatia.
Kushiriki mapenzi ya jinsia ni hatia kisheria katika mataifa mengi ya Afrika na hukumu yake huwa ni kifungo grezani.
Kupigwa risasi
"Jaji
alitoa hukumu ya wanaume hao watatu hadharani na kuwapata na hatia.
Walipigwa risasi na kuawa katika mji wa Buale," Sheikh Abdalla,
aliliambia shirika la habari la Reuters.
Afisa wa serikali ya Somalia amesema kesi yoyote juu ya mapenzi ya
jinsia moja nchini Somalia, taifa lenye idadi kubwa ya waumini wa dini
ya Kiislamu, inafaa kushughulikiwa kwa mujibu wa Sharia.
Hata hivyo hakufafanua jinsi sheria hiyo itakavyotekelezwa.
COMMENT AND SHARE.........................!!!!!!!!!!!
Share And Comment Bellow On What You Think About This Post!!!
Comments
Post a Comment
Welcome.......
What are you thinking of....!!