Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment and dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment and dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment., dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment., dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!!

Namna au Jinsi ya Kuzuia Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI..:;

Kondom.jpg              Ni muhimu jamii ielimishwe umuhimu wa kupima afya zao na kuchukua hatua zinazostahili. 
 
Jinsi ya kuzuia maambukizi ya VVU yanayotokana na kujamiiana 
Kutokujamiiana kabisa (kugunga) 
Kuwa na mpenzi mmoja mwaminifu na asiye na uambukizo 
Kujamiiana kwa kutumia kondomu ya kike au ya kiume kwa usahihi na wakati wote 

Jinsi ya kuzuia maambukizi kwa mtoto mchanga 
Wanawake wajawazito wahudhurie kliniki ili kupima na kufahamu  afya zao. 
Washauriwe vilevile wahudhurie na waume au wenzi wao ili  kupata unasihi wa kupima VVU. 
Wanawake wajawazito wanaobainika kuwa na VVU na wenzi wao wa kiume, wapewe ushauri nasaha (unasihi) kuhusu uamuzi wa kunyonyesha au lishe mbadala kwa mtoto mchanga
Wanawake wajawazito wanaobainika kuwa na VVU wapewe dawa  za kuzuia maambukizi kwa mtoto. Familia ambayo mama atakuwa amebainika kuwa na virusi vya UKIMWI wakati wa ujauzito, ipewe rufaa ili kuendelea na huduma au matibabu mengine kwa waishio na virusi vya UKIMWI. 
Wanawake wote hasa wale waliobainika kuwa na VVU washauriwe kujifungulia kwenye vituo vya afya. Wakina mama waliobainika kuwa na VVU ambao wamejifungulia nyumbani wapeleke watoto kliniki ndani ya masaa 48 baada ya kujifungua. 
Jamii kwa ujumla ishirikishwe kutoa msaada wa hali na mali kuwawezesha wakina mama walioambukizwa VVU kutimiza masharti  ya kuzuia mambukizi kwa mtoto. 
Jinsi ya kuzuia maambukizo ya VVU wakati wa kutoa huduma 
Ni muhimu watoa huduma wawe waangalifu wakati wa kuwahudumiawagonjwa na kuzingatia mambo yafuatayo:
Endapo mtoa huduma ana michubuko, majeraha au vidonda mikononi lazima vifungwe vizuri kwa kitu kisichopitisha majimaji kama plasta au kuvaa mipira ya mikononi  wakati wa kumhudumia     mgonjwa Kabla ya kugusa nguo au vifaa vyenye damu, matapishi, mkojo au kinyesi cha mgonjwa ni muhimu mtoa huduma kuvaa mipira ya mikononi na mgonjwa aelezwe sababu ya kufanya hivyo. 
Nguo au vifaa vyenye damu ya mgonjwa au majimaji mengine kutoka kwenye vidonda viwekwe kwenye maji ya moto yanayochemka kwa dakika 20-30 au vilowekwe kwenye JIC kwa dakika 20-30 kabla ya kufua/kuosha.  
Mhudumu afue/asafishe vifaa hivyo akiwa amevaa mipira ya mikononi  
Vitambaa vilivyofunga vidonda, mipira ya mkononi ilivyotumika kwa kumhudumia mgonjwa wa UKIMWI viteketezwe kwa moto.Vifaa vingine visivyochomeka vitumbukizwe katika choo cha shimo. 
Mhudumu avae mipira ya mikononi wakati wa kumbeba mgonjwa mwenye vidonda. 
Vifaa vyenye ncha kali vilivyotumika wakati kwa kumhudumia mgonjwa wa UKIMWI na ambavyo vinaweza vikatumika tena vilowekwe kwenye JIC halafu vichemshwe.  Vile ambavyo havitatumika tena, vitumbukizwe kwenye choo cha shimo. 
Mhudumu aoshe mikono kwa sabuni kabla na mara baada ya kumhudumia mgonjwa.    





COMMENT AND SHARE............................!!!!!!!!!!
Share And Comment Bellow On What You Think About This Post!!!

Comments

Facebook Twitter Youtube