
Rapa Joh Makini ameufungua mwaka 2017 kwa kutoa ngoma matata inayokwenda
kwa jina la 'Waya' lakini maswali mengi ni kwamba vipi ile collabo yake
aliyoifanya na msanii Davido kutoka Nigeria?
Camera
ya eNewz ya EATV ilimtafuta na kutaka kujua kulikoni..! ambapo
alifunguka na kusema kuwa collabo hiyo bado ipo palepale na kwamba
inasubiri wakati wake ukifika, itakuwa hewani.
Alisema kwa kawaida katika kamati yake
huwa wanakaa na kuangalia ni ngoma gani itoke na kwa wakati gani ambapo
kamati hiyo ndiyo iliyoamua ngoma ya Waya itoke sasa badala ya ile
aliyofanya na Davido.
“Waya nahisi ni wimbo ambao nimeamua
kuutoa sasa na siyo huo tu nina ngoma nyingi sana nzuri ambazo ziko
ndani kwahiyo kikubwa tunachoangalia ni timing tu, kwa hiyo sasa hivi
nimeona nitoe waya kwanza na siyo kama collabo na Davido haipo, ipo na
imeshakamilika lakini muda ukifika nitaitoa na siyo Davido tu, nina
ngoma pia na YCEE na Falz na nyingine nyingi kali sana, mimi na team
yangu tunakaa na kuangalia kwa sasa ni ngoma gani itoke na sasa tuliona
Waya utatikisa ndiyo maana tumeutoa”
Pia Joh Makinni aliongeza kwa kusema
kuwa kila muziki aliorekodi ni mkubwa kwa hiyo mashabiki bado waendelee
kukaa tayari na kuendelea kusapoti muziki wake.
COMMENT AND SHARE........................!!!!!!!!!
Share And Comment Bellow On What You Think About This Post!!!
Comments
Post a Comment
Welcome.......
What are you thinking of....!!