Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment and dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment and dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment., dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment., dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!!

Je, Muitaliano Atamrithi Arsene Wenger Kuinoa Arsenal?

Arsene Wenger                
Inadaiwa Arsenal wapo kwenye mazungumzo yaliyochangamka na meneja mpya kuchukua nafasi ya Arsene Wenger msimu ujao
Bosi huyo wa Kifaransa amekuwa akiinoa Arsenal kwa muda wa zaidi ya miaka 20 sasa, na amewaongoza katika nyakati ngumu za uchumi huku akiwahakikishia nafasi yao katika michuano ya Ulaya.
Wenger kwa umaarufu ameiongoza timu yake, ikimaliza msimu bila kufungwa hata mechi moja katika msimu wa 2003-01 Ligi kuu, lakini licha ya hatua hiyo, amekuwa akishambuliwa na mashabiki wanaotaka mafanikio miaka ya hivi karibuni.
Makundi hayo ya mashabiki yamejaribu kupinga yakitaka mabadiliko katika klabu hiyo, wakati mabango yakimtaka Mfaransa huyo kuachia ngazi yalionekana kuzagaa katika uwanja wa Emirates.
Mkataba wa Wenger unakaribia kufika mwisho msimu ujao wa majira ya joto, na kukiwa hakuna dalili ya mkataba mpya, klabu inafanya mchakato wa kutafuta kocha mpya.
Massimiliano Allegri kwa sasa anadaiwa kuwa kwenye mazungumzo yaliyochangamka na uongozi wa klabu kuchukua dili la kuinoa Arsenal.
 Allegri Juventus
Muitaliano huyo ametwaa taji la Ligi ya Italia akiwa na Juventus katika misimu mitatu tangu alipochukua mikoba ya bosi wa sasa wa Chelsea Antonio Conte aliyeondoka klabuni hapo kuinoa timu ya taifa ya Italia.
Bosi huyo wa Juve inaaminika kuwa anatamani sana kutua Uingereza kushindana na Muitaliano mwenzake lakini makubaliano kwa ajili ya kibarua kipya hayajafikiwa.
Meneja wa Leipzig Ralph Hasenhuttl na kocha wa Bournemouth Eddie Howe pia ni waalimu wanaopewa nafasi kubwa kumrithi Wenger.
Je! Allegri ni mtu sahihi kurithi nafasi ya Wenger?    




COMMENT AND SHARE..............!!!!!!!
Share And Comment Bellow On What You Think About This Post!!!

Comments

Facebook Twitter Youtube