Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment and dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment and dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment., dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment., dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!!

Homa ya Ndege Yagunduliwa Huko Uganda..:;

Aina ya Bata wa kufugwa ambao wanaaminika kuambukizwa homa ya Ndege          
Serikali ya Uganda, imethibitisha kuwepo kwa ugonjwa wa homa ya ndege katika maeneo karibu na fuo za Ziwa Victoria.
Virusi hivyo vimethibitishwa kwa ndege wanaohama, bata wanaofugwa na kuku.
Wakuu sasa wametoa tahadhari kwa jamii za maeneo hayo kuhakikisha kuwa ugonjwa huo hausambai na kuwaambukiza watu. Mwaandishi wa BBC nchini Uganda, Catherine Byaruhanga. Anasema kuwa ripoti za awali za ndege waliokufa zilianza kutolewa mwanzo tu wa mwaka huu.
Jamii za maeneo hayo, wamesema kuwa, walizipata mizoga ya ndege wengi waliokuwa wakihamia Uganda wakati wa majira ya baridi katika maeneo ya kaskazini mwa dunia.
Majaribio kadhaa yaliyofanywa na wataalamu, yalithibitisha kuwa, ndege hao walifariki kutokana na maradhi ya Highly Pathogenic Avian Influenza au bird flu, yaani homa kali ya ndege kama inavyofahamika.
Chembechembe zilizokusanywa kutoka kwa mizoga ya bata wa kufugwa na kuku, katika Wilaya moja ya eneo hilo karibu na Ziwa Victoria upande wa Uganda, zilithibitisha hilo.
Hakuna taarifa zozote za ugonjwa huo kuambukiza binadamu, na serikali ya Uganda imesema kuwa, inawashauri jamii za maeneo hayo kuhusu namna ya kujikinga kupatwa na ugonjwa huo na mbinu za kuzua kuzambaa zaidi.
Vikosi vya majanga ya dharura vimetumwa huko ili kukusanya mizoga ya ndege hao waliokufa.
Hii ni mara ya kwanza kwa mlipuko wa ugonjwa huo kutokea nchini Uganda, lakini mamlaka kuu ya nchi hiyo, imefumbua mbinu mpya ya kukabiliana kwa haraka namna ya kushughulikia majanga ya dharura ya kiafya, hasa kufuatia visa vya ugonjwa hatari wa Ebola.    



COMMENT AND SHARE.................!!!!!!!!
Share And Comment Bellow On What You Think About This Post!!!

Comments

Facebook Twitter Youtube