Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment and dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment and dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment., dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment., dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!!

Zitto Kabwe Afunguka yake Kuhusu Operesheni UKUTA....Adai ni Haki yao Kuandamana

                     Wakati viongozi wa dini wakiendelea na jitihanda za kusaka suluhu kati ya upande wa Serikali na Chadema kuhusu namna ya kuzuia kwa amani kufanyika kwa Operesheni ya chama hicho iliyopewa jina la UKUTA, Septemba 1, Kiongozi Mkuu wa Chama Cha ACT-Wazalendo Zitto Kabwe ametoa maoni yake.

Zitto ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Mjini amesema kuwa haoni haja ya kufanyika kwa vikao hivyo vya kusaka maridhiano kwani Chadema wanachotaka kufanya kiko kikatiba.

“Sioni ni kwanini tunahangaika na vikao vya maridhiano na tahariri nyingi kuhusu shughuli ya CHADEMA kufanya operesheni yao ya UKUTA. Kuandamana ni Haki ya KIKATIBA. Tuache watu watimize Haki yao Kwa amani. Kuzuia watu kufanya jambo lao la kikatiba ndio kuvunja amani. Wanaotaka kuandamana waandamane na wanaotaka kufanya Kazi zao nyingine tuendelee na Kazi zetu. Kwanini kutekeleza Haki ya kikatiba iwe ni kuvunja amani? Kwanini?,” Zitto ameandika kwenye ukurasa wake wa Facebook.

Hata hivyo, vikao vya maridhiano vinavyoendelea tayari vimeonesha kuzaa matunda kwenye suala la mgogoro wa Bunge ambapo wabunge wa vyama vya upinzani wameridhia kurejea Bungeni katika vikao vitakavyoanza mapema mwezi ujao.

Serikali imeendelea kuwaonya watu wote wanaopanga kuandamana Septemba 1 huku viongozi wa Chadema wakisisitiza kuwa siku hiyo watafanya maandamano kama walivyopanga.

Hali hiyo imepelekea kumtoa hadharani Kingunge Ngombale Mwiru ambaye ameomba marais wastaafu kumshauri Rais Magufuli ili kuruhusu Serikali kukaa na Chadema kusaka muafaka wa masuala ya kisiasa nchini.
Share And Comment Bellow On What You Think About This Post!!!

Comments

Facebook Twitter Youtube