Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment and dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment and dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment., dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment., dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!!

Rage acharuka, Hans Pop amjibu

           
SAKATA la kudakwa kwa viongozi wa Simba na Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru), limechukua sura mpya baada ya viongozi wa klabu hiyo kuanza kushikana uchawi, huku Rage akimpa siku saba Zakaria Hans Pope kumuomba radhi.
Rage amevunja ukimya na kutaka kuombwa radhi kufuatia kauli ya Mwenyekiti huyo wa Kamati ya Usajili ya Simba, kudai kuwa fedha za mshambuliaji Mbwana Samatta aliyeuzwa TP Mazembe zilipitia kwenye akaunti ya mke wa Rage wakati akiwa Mwenyekiti wa klabu hiyo.
"Nadhani mtu mwendawazimu tu anaweza kufanya hivyo, mke wangu hana hata akaunti…Kama anajua akaunti ya mke wangu aipeleke Takukuru aje achukuliwe, mimi mtu makini, nimeshaongea na wakili wangu amshughulikie akishindwa kuniomba radhi ndani ya siku saba. La sivyo suala hili litaenda mahakamani," alisema Rage.
"Waache kuweweseka kinachozungumzwa ni fedha za Okwi sio fedha za Samatta, suala hili kwa sasa lipo kwenye vyombo vya sheria, waachie vifanye kazi yao kwani mpaka sasa ni tuhuma tu, hata wakipelekwa mahakamani bado itakuwa ni tuhuma na wakae wakijua hii ni Awamu ya Rais wa Tano, haina msalie Mtume, ni kumbakumba tu, ” alisema Rage.
Kauli ya Rage imekuja baada ya Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zakaria Hans Pope kudai kuwa Rage ameshikia bango suala hilo wakati yeye fedha za Samatta zilipita kwenye akaunti ya mke wake.
“Rage anapiga kelele sana pesa za Okwi yeye za Samatta zilipitia kwenye akaunti ya mkewe na hakupigiwa kelele, “alisema Pope na kuongeza:
“Kuhamisha pesa sio kosa la jinai akaunti ilifungiwa huwezi kutumia pesa yoyote hata kama kodi ni kidogo ya kilichopo. Kipindi hicho hapakuwa na kodi yoyote inayodaiwa kwa hiyo hapakuwa na kosa lolote.”
“Hizi ni fitina tu kwa nini itumike Takukuru?” alihoji Pope. Takukuru ilimshikilia Aveva kwa tuhuma za utakatishaji fedha zilizolipwa na Etoile du Sahel ya Tunisia za malipo ya mauzo ya Mganda Emmanuel Okwi ambaye zililipwa kwenye akaunti ya klabu ya Simba mwezi Machi mwaka huu na uchepushaji wa fedha kutoka kwenye akaunti hiyo ya Wekundu wa Msimbazi ndipo ulipoanzia.
Taasisi hiyo bado inaendelea na uchunguzi wa miamala ya kifedha kwenye akaunti za viongozi mbalimbali wa Simba ikiwemo akaunti binafsi ya Rais huyo wa Wekundu wa Msimbazi kwa kile walichodai kuwa kuna miamala ya kutia shaka ikiwemo dola 62,000 zilizolipwa kwenye Benki ya Hong Kong na dola 19,000, ambazo zilifanya malipo mbali mbali kwenye akaunti za watu binafsi.
Katika mkutano huo uliofanyika hivi karibuni uliwasilisha bajeti kivuli ya mwaka 2016/2017 ukitaka wajumbe ambao ni wanachama kuipitisha bajeti hiyo, kitendo ambacho kiliwachefua wanachama ambao hawakuijadili bajeti hiyo na badala yake walipiga kelele za mabadiliko na kutaka timu akabidhiwe mfanyabiashara Mohamed Dewji maarufu ‘Mo’.
Akizungumza la kuwachomea utambi Rage alisema “nilizishikia bango kwa vile nilishutumiwa sana kuwa mimi zile hela nimekula wakati haikuwa hivyo, walinitia doa sana sasa wanaumbuka”.
Simba ilikuwa inaidai Etoile dola 300,000 sawa na Sh milioni 600, lakini pia imelipwa dola 19,000 kama fidia ya usumbufu wa kufuatilia deni hilo.
Share And Comment Bellow On What You Think About This Post!!!

Comments

Facebook Twitter Youtube