Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment and dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment and dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment., dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment., dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!!

Mfalme wa JAPAN atangaza kung’atuka madarakani

Mfalme wa JAPAN AKIHITO ameeleza mpango wake wa kutaka kung'atuka kutokana na umri mkubwa aliokua nao                             
AKIHITO mwenye miaka 82 amesema ana wasiwasi kuwa huenda ikawa vigumu kwake kutekeleza majukumu yake kutokana na kuzorota kwa afya yake.
Akihutubia taifa hilo kupitia runinga, amesema kulikua na vipingamizi katika mpango wa kupunguza majukumu ya mfalme kama nembo ya taifa.
Watu wengi wamekua na mitazamo tofauti kuhusu taarifa hiyo lakini hata hivyo hatua hiyo inahitaji mabadiliko ya sheria ya JAPAN ambapo kwa sasa hakuna nafasi kisheria inayomruhusu mfalme kuondoka madarakani.
Waziri Mkuu wa JAPAN, SHINZO ABE, amesema atatathmini kwa makini matamanio ya mfalme huyo.
Akizungumza muda mfupi baada ya hotuba ya Mfalme AKIHITO Waziri Mkuu amesema atazingatia nini kinachoweza kufanywa na serikali kwa ajili ya Mfalme. Mfalme AKIHITO amekuwa madarakani tangu mwaka 1989 baada ya kifo cha baba yake, HIROHITO.
Share And Comment Bellow On What You Think About This Post!!!

Comments

Facebook Twitter Youtube