Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment and dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment and dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment., dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment., dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!!

KWA NINI UPWEKE NI HATARI KWA AFYA?

KWA NINI UPWEKE NI HATARI KWA AFYA?:;           


          Kuwa mpweke kwaweza kuwa hatari kwa afya mara mbili zaidi ya hatari itakanayo na kuwa na uzito mkubwa, kutokana na utafiti uliofanyika, mtu anapohisi kutengwa, au kutengwa na jamii yake inakuwa hatari sana husani mtu huyo anapokuwa amefikisha umri wa kati.

Utafiti uliofanyiwa kwa watu walio na umri zaidi ya miaka 50 umegundua kuwa watu waliokuwa wapweke walikuwa katika hatari ya kufa mapema mara mbili zaidi ya wale waliokuwa wamezungukwa na jamii zao,
matokeo hayo yalionekana baada ya miaka mingi ya utafiti huo.
Katika utafiti huo, ulinganisho wa wastani wa idadi ya watu waliofanyiwa utafiti, wale waliosema walikuwa wapweke walikuwa na asilimia 14 ya hatari ya kufa mapema. Kiwango hicho ni mara mbili ya hatari itokanayo na kuwa na uzito mkubwa kati ya hao waliofanyiwa utafiti.
Utafiti uliofanyika kwa wale walio wazee huko Uingereza katika mwaka wa 2012 wanasayansi waligundua kuwa, wazee wengi walijihisi wapweke na waliotengwa muda wote, na hali hiyo ya kutengwa iliongezeka zaidi wakati wa mwisho wa wiki(weekend) na nyakati za usiku.
Tafiti nyingi zilizofanyika zimeonyesha kuwa, upweke unahusiana moja kwa moja na magonjwa  kama shinikizo la damu, udhaifu wa kinga ya mwili, hatari kubwa ya kupata msongo wa mawazo, shambulizi la moyo na kiharusi.
“Watu huwa na mtazamo usio wa kawaida kuhusu kustaafu kazi. Wengi hufikiri kustaafu  ni kutengana na marafiki, familia na watu wengine na kutafuta sehemu tulivu za kumalizia maisha kwa furaha. Lakini inawezekana hilo sio jambo zuri “ mwandishi wa kitabu cha upweke (Loneliness) John Cacioppo alisema.
Watu ambao wataendelea kuwa karibu na wafanyakazi wenzao,familia zao, marafiki na ndugu wengine baada ya kustaafu wanazidi kuwa wachangamfu na wasio na upweke. Kuwa na muda wa kufurahia maisha na tumia nyakati za furaha na familia na marafiki. Watu wasio wapweke ni wale walio karibu na familia, marafiki na jamaa.
Share And Comment Bellow On What You Think About This Post!!!

Comments

Facebook Twitter Youtube