Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment and dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment and dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment., dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment., dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!!

Kigwangalla alaumu wanachama Yanga

           
NAIBU Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt Hamis Kigwangalla amesema wanachama wa Yanga wanapaswa kulaumiwa kwa kutomtendea haki mwenyekiti wao Yusuf Manji, baada ya kushindwa kumuuliza maswali.
Kauli hiyo ya Kigwangala imekuja siku chache baada ya mkutano mkuu wa dharura wa Yanga kukubali kumkodisha Manji timu yao kwa miaka 10.
Akizungumza juzi baada ya mchezo wa kirafiki kati ya Simba na AFC Leopard, Dkt Kigwangalla alisema wanachama hawakumtendea haki kwani walipaswa kumuuliza Manji maswali ambayo yangetoa mustakabali wa klabu yao.
“Manji anapaswa kuweka wazi ni kwa nini apewe asilimia 75 na sio 25 ya faida itakayopatikana na ni kwa nini atake kukodishwa miaka 10 na si miwili au mitatu na kwa gharama gani?”Alihoji. “Naona mwanga kwa upande wa Simba ambayo inaenda kwa mfumo wa Kampuni na kuuza hisa, ila ninachowashauri Mo Dewji (Mohamed) apewe asilimia 40 na si asilimia 51,hii itapunguza kumfanya atoe maamuzi yake peke yake. “
Asilimia zilizobaki ziende kwa wanachama ili nguvu ibaki kwa watu wengi zaidi na si mtu mmoja awe na nguvu.
“Siwaungi mkono Yanga hata kidogo, kumpa mtu mmoja timu kwa miaka 10 bure, nafurahi wanavyofarakana kwa vile mimi ni shabiki wa Simba, waache wavurugane sisi tunaelekea kwenye mafanikio. “Manji amekuwa na sauti Yanga kuliko mtu yeyote, amewashika masikio anachotaka yeye ndio hicho hicho, ana sauti kuliko mtu yeyote, anafukuza watu, anafanya anavyotaka, hii si sawa,” alisema Dkt Kigwangalla.
Kwa upande wa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alipoombwa kutoa maoni yake juu ya hilo alisema: “Unataka kujua kwa nini Tanzania ni masikini pamoja na utajiri mkubwa wa maliasili tulizonazo? Soma mkataba wa Yanga wanaosaini”.
Hata hivyo, Mjumbe wa Bodi ya wadhamini wa klabu hiyo, Francis Kifukwe alisema wao sio wajinga wakubali kumpa Manji timu miaka 10 bila kufuata mambo ya msingi na kwamba kuna mambo mengi watayafuatilia na kutoa tamko siku yoyote kuanzia leo.
Habari ambazo HabariLeo imezipata zinasema kuwa bodi ya wadhamini ilitarajiwa kukutana jana kupitia maombi ya Manji.
“Baraza litapitia kipengele kimoja baada ya kingine kuangalia klabu itakavyonufaika, vigezo vitakavyotumika katika kumkodisha, kabla ya kuridhia ombi la Manji,” alisema mmoja wa viongozi wa klabu hiyo.
Share And Comment Bellow On What You Think About This Post!!!

Comments

Facebook Twitter Youtube