Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment and dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment and dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment., dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment., dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!!

Kampeni ya matumizi sahihi ya mitandao yaja,

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA imepanga kuanzisha kampeni ya kuongeza ufahamu kwa watumiaji wa mitandao ili watanzania waepukane na mkono wa sheria ya makosa ya mitandao inayoelezwa kuwa kikwazo cha uhuru wa kujieleza             
Kampeni hiyo imekuja mahsusi kwa ajili ya kuimarisha usalama katika matumizi ya mitandao kipindi hiki ambacho kumekuwa na madai ya watu wengi kukiuka sheria ya mitandao.
TCRA imeamua kuja na kampeni hiyo kutokana na watanzania wengi kukosa ufahamu juu ya sheria ya mitandao hali inayochangia uwepo wa ongezeko la ukiukwaji wa sheria hiyo na kusababisha uwepo wa migogoro.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TCRA James Kilaba amekiri kumekuwa na ongezeko la watumiaji wa wavuti jambo ambalo linawasukuma kutoa elimu kwa rika zote ili wafahamu matumizi sahihi ya mitandao.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TCRA pia ametumia nafasi hiyo kubainisha masuala muhimu ya kuzingatia wakati wa kutumia intaneti au mitandao.
Kampeni hiyo inatarajiwa kudumu kwa kipindi cha miezi mitatu na itaendeshwa kwa kutumia mitandao.
          



COMMENT AND SHARE..................................
Share And Comment Bellow On What You Think About This Post!!!

Comments

Facebook Twitter Youtube