Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment and dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment and dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment., dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!! Welcome to VIVAX MEDIA, feel free to Comment., dont forget to Share (also please Click on the YOUTUBE, YOUTUBE, YOUTUBE button above/bellow the page).....!!

JE NI UMRI GANI MUAFAKA WA KUPIMA SARATANI YA TEZI DUME?

JE NI UMRI GANI MUAFAKA WA KUPIMA SARATANI YA TEZI DUME?:;      

                   Saratani ya tezi ya prostate(tezi dume) ni ile ambayo seli zisizo za kawaida hukua katika tezi ya prostate iliyopo katika mfumo wa uzazi wa mwanaume. Kwa walio wengi, ukuaji wa saratani hii huwa ni wa taratibu ingawa kwa wengine yaweza kukua kwa haraka. Saratani yaweza kusambaa katika sehemu nyingine za mwili,hususan katika mifupa na tezi zinazo husika na kinga ya mwili (lymph nodes). Mara nyingi saratani ya tezi ya prostate huwa haionyeshi dalili yeyote katika hatua za awali. Saratani hii imeonekana  kuwaathiri zaidi wanaume wenye asili ya Afrika na Caribbean lakini haijulikani ni kwa sababu gani.

Dalili za saratani hii hutofautiana kati ya mtu mmoja hadi mwingine; baadhi ya wanaume huwa hawaonyeshi dalili hadi saratani inapokua baada ya mwaka mmoja, na dalili zinapojitokeza huwa kama ifuatavyo:
  • Kukojoa mara kwa mara
  • Mkojo unaokatika wakati wa kukojoa.
  • Mkojo kutoka kwa shida unapoanza kukojoa.
  • Damu katika mkojo au katika majimaji yanayobeba mbegu za kiume.
  • Maumivu wakati wa kukojoa au kujamiaana.
  • Maumivu makali ya mgongo, kiuno mapaja, hususan pale ugonjwa unakua umesambaa katika ogani nyingine za mwili.
Kuna aina mbili za magonjwa ambazo husababisha dalili zinazofanana na saratani ya tezi ya prostate. Ugonjwa wa kwanza ni ule ambao tezi ya prostate huongezeka ukubwa isivyo kawaida, lakini ukuaji huu hausababishwi na saratani (kitaalam hujulikana kama benign prostatic hyperplasia- BPH). BPH husababisha dalili kwa kuongeza mkandamizo katika kibofu cha mkojo, mrija wa kutoa mkojo kutoka katika kibofu, au kibofu pamoja na mrija kwa pamoja na ugonjwa huwapata wanaume wenye umri mkubwa. Ugonjwa wa pili ni ule ambao husababishwa na uambukizi katika tezi ya prostate na kupelekea uvimbe wa tezi hii. Magonjwa haya yote hutibika na BPH wakati mwingine huitaji matibabu ya upasuaji.
Watafiti wanashauri watu kutumia vyakula kama matunda na mboga mboga kwa kuwa vyakula kutokana na wanyama kwa wingi, kama nyama zenye mafuta mengi ni vichochezi vinavyoweza kusababisha mtu kupata saratani ya tezi ya prostate, ingawa tafiti zaidi zinaendelea kujua ni kwa jinsi gani vyakula hivi vinachochea mtu kupata ugonjwa huu.
Je saratani ya tezi dume yaweza kugundulika mapema?
Ijapokuwa upimaji wa saratani ya tezi dume huwa haufanyiki mara kwa mara na huwa hamna kampeni za kuhamasisha upimaji kama ilivyokuwa kwa saratani ya matiti, lakini wataalam wanaohusika na magonjwa ya saratani wanashauri upimaji wa saratani kwa makundi yafuatayo:
  • Wanaume wenye miaka 50 na wanataka kuongeza umri wa kuishi.
  • Wanaume wenye miaka 45 wa asili ya Afrika wenye baba au kaka ambao walipatikana na saratani ya tezi ya kiume kabla ya miaka 65.
  • Wanaume wenye miaka 40 ambao ndugu wa karibu (baba, kaka au kijana) walipatikana na saratani ya tezi ya prostate katika umri mdogo.
Vipimo vya awali kabisa ili kugundua ugonjwa huu hujulikana kama PSA (prostate specific antigen) na kingine ni DRE (digital rectal examination) ambapo daktari hutumia glove kwa kutumia kidole kupitia njia ya haja kubwa kupapasa uvimbe katika tezi ya prostate. PSA ni kwa kupima damu kuangalia kiwango cha antigeni za prostate. Daktari na mgojwa hutakiwa kuwa makini kuhusu majibu ya vipimo hivi kwa kuwa ni vipimo vya awali kabisa na matokeo yaliyo chanya hayamaanishi mojakwamoja kuwa mgonjwa anayo saratani. Daktari atamsaidia mgonjwa kuamua ni nini maana ya vipimo vyote vya PSA na DRE na kuamua vipimo vitakavyofuata baada ya vipimo hivyo.
 
Kama daktari wako ataamua kuwa vipimo vya PSA na DRE vimeonyesha saratani ya prostate, kipimo kitakachofuata ni upimaji wa tishu kutoka katika tezi ya prostate ( kitaalam kama biopsy). Kipimo hiki hufanyika kwa kuchukua tishu kwa kutumia sindano maalum, ambapo tishu hizi huchunguzwa kwa kutumia darubini ili kuangalia uwepo wa seli za saratani katika tezi ya prostate.
Share And Comment Bellow On What You Think About This Post!!!

Comments

Facebook Twitter Youtube